Mwongozo wa usimamizi shirikishi unaohusisha jamii ya wavuvi wa pwani ya bahari ya hindi
Mwongozo huu umeandaliwa kwa ajili ya kuanzisha usimamizi shirikishi wa
raslimali za pwani na bahari unaohusisha jamii. Kitabu hiki kimeandaliwa kwa
ajili ya kuwafundisha waraghabishi na baadae kitumike kutoa mafunzo kwa
jamii.
Mwongozo huu umegawanyika katika masomo sita ambayo ni Sera na Sheria ya
Uvuvi; Usimamizi wa Shughuli za Uvuvi; Usimamizi shirikishi unaohusisha
jamii; Utawala bora; Utatuzi wa migogoro na Viashiria.
Wakati wa kutoa mafunzo kwa waragabishi ni lazima kufundisha masomo yote sita
ili wafahamu maeneo ya msingi.
Baada ya mafunzo wahitimu watawaelimisha jamii ya wavuvi ili waanzishe
usimamizi shirikishi wa raslimali za pwani na bahari unaohusisha jamii katika
vijiji vyao. Pia, wahitimu (waraghabishi) watatakiwa kutumia elimu
waliyoipata kuwafundisha Viongozi wa Serikali za Vijiji, Maafisa Watendaji wa
Vijiji, Maafisa Watendaji wa Kata na viongozi wengine wa ngazi za Tarafa na
Wilaya.
Language:
Swahili
Document date:
2009-03



